Jumatano, 29 Aprili 2015

UPENDO


Jina la Yesu  lipewe  sifa………..

Nakupenda sana msomaji wa ukurasa huu wa NUKUU ZA MUNGU
Na wewe ni mtu wa pekee sana kwangu, natambua uwepo wako katika kushirikiana nami kutangaza Neno la Mungu.

Hivyo basi nahitaji kushirikiana na wewe leo neno linahusu UPENDO!
Upendo huwezi kutokea pasipo kuonesha ama kutambua thamani ya kile ukipendacho. Hivyo upendo ni hali ya kuonesha kujali, kuthamini kitu ama MTU.

Upendo ni agizo tulilopewa na Mungu, na kuthibisha hili Mungu alianza kutupenda sisi. “ Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe pekee, ili kila mtu mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”. Yohana 3:16

Hii ni dhahili kabisa kuwa UPENDO ni kitu chenye thamani kinachoweza hata kugharimu uhai wa mtu. Lakini basi, ni nani awezae kuufuata ule UPENDO aliotuonesha bwana Yesu kwa kukubali kujitoa uhai wake kwa ajili ya maisha yetu? Jibu ni hakuna……….sio mimi nasema bali  “Hakuna aliye na upendo mwingi kama huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.” Yohana 15:13

Hivyo basi Mungu kwa kutambua madhaifu yetu na mapungufu yetu ametuagiza kupendana sisi kwa sisi, kuchukuliana mizigo, kusaidiana matatizo kuona kila mmoja anathamani kwa mwenzie, na hapo tutakuwa tunampenda Mungu. Kwani katika kitabu cha 1 Yohana 4:21 tunaagizwa “Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye mungu, ampende na ndugu yake.” Hii inamaanisha kuwa mtu hawezi kumpenda Mungu kama hajampenda ndugu yake kwanza.

Na humohumo kwenye biblia inaongeza kwa kutuulizaa, Kama unaamchukia ndugu yako unaye muona, Je,  Mungu usiye muona utampendaje? Hivyo upendo uanze kwetu sisi wenyewe.

Warumi 12:9, inasisitiza kuwa upendo wetu usiwe wa kinafki, tupendane UPENDO wa kweli kwani pendo la kweli lina faida, linajenga Amani,  linaondoa Uongo, linaleta Baraka, LINAONDOA DHAMBI.
Na katika UPENDO tutafika mbinguni, kwani utatuweka karibu na Mungu na kutuweka mbali na dhambi.

Siku njema, na Mungu akubariki kwa Upendo wake wa kweli.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni