Habari za wakati
huu, ndugu msomaji katika ukurasa huu wa
NUKUU ZA MUNGU.
Leo naanza kwa maswali
mawili matatu hivi;
1.
Je unajua mahali sahihi pa kueleza shida
zako?
2.
Je ni nani wakumueleza shida zako?
3.
Ipi ni njia sahihi ya kumaliza shida
zako?
Wengi wamekuwa wakikosa
majibu ya maswali haya, na kuanza kuhamisha imani zao kwa kupeleka shida zao
kwa ndugu, majirani na wengine hata kudiriki kwenda kwa waganga wakiamini
kupata suluhisho ya maswali yao.
Lakini leo nataka
kuwapa jibu lililo sahihi ambapo tukianza kwa kuangalia katika kitabu cha Marko
11:24 “Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, amini ya kwamba
mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.”
Hivyo basi ndugu
msomaji tunaelezwa kuwa kuwa NJIA iliyo sahihi yakueleza shida, mahitaji na
matatizo yetu ni kwa njia ya MAOMBI, KUFANYA SALA kwa baba yetu yetu aliye
MBINGUNI. Na si kama vile watu wanavyofikiri kueleza matatizo yao kwa ndugu ama
kwa majirani na wengine kwenda kwa waganga.
Hiyo sio njia sahihi
ndugu zangu, leo tunajifunza hili ili tupate kujua kuwa Mungu ndio msuluhishi
wa matatizo yetu na sio mtu mwingine yeyote.
Mathayo 7:7 “Ombeni
nanyi mtapewa, tafuteni mtaona, bisheni nanyi mtafunguliwa.”
- · Wewe unaomba kwa nani?
- · Unatafuta kwa nani?
- · Unabisha kwa nani?
Ili kupata muafaka wa mahitaji yako?
Mungu wetu hashindwi na
jambo Bwana, ebu nenda wazungu wanasema direct kwake mueleze mambo yako, muombe
mahitaji yako, tafuta kwake kilicho chako, kapate haki yako.
Zungumza naye kwa
upole, kuwa na ujasiri katika kumueleza mambo yako, naye atakujibu. Halleya!!!!!!!!!!!!!!!!!
Wengi wetu tunaharibu
wenyewe, pasipo kujua. Tunahitaji Mungu atujibu mahitaji yetu huku mioyoni
mwetu tumebeba mizigi isiyo mpendeza Mungu, TUJIULIZE SISI KAMA WANADAMU NA KAMA MZAZI,
MTOTO WAKO AMEKUKOSEA, JE MTOTO ATAPATAJE UJASIRI WAKUELEZA SHIDA ZAKE KWA
MZAZI?
Na sisi kwa Mungu wetu
ni watoto wake, tunapomkosea hukasirika sana. Hivyo tunakiwa kuomba msamaha ama
kutubu dhambi zetu kabla ya kueleza shida zetu.
NDUGU MSOMAJI
TUNACHOTAKIWA KUFAHAMU NI NAMNA YA KUENDENDA SAWASAWA MBELE ZA MUNGU, NAYE NI
MWEMA KATIKA MAISHA YETU, ANASIKILIZA NA KUJIBU MAOMBI YETU. HIVYO
TUJINYENYEKEESHE MBELE ZAKE NAYE ATATUJIBU.
BASI NIKUTAKIE WAKATI
MWEMA WENYE BARAKA ZA MUNGU…………….
NATUKUTANE SIKU
NYINGINE
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni