Jumatano, 29 Aprili 2015

MUNGU HUPENDA SIFA


Bwana Yesu apewe sifa,

Leo ni siku nyingine iliyo njema na ya kumpendeza Mungu.

Tumekuwa tukijifunza mengi sana yamuusuyo Mungu wetu, na leo tutaeenda kufahamu nini kuhusu SIFA kwa Mungu wetu.

SIFA ni kitendo cha kumtukuza, kumfanyia shangwe, kumuinua, kumshukuru kwa kutambua yale makuu aliyonayo na aliyokutendea wewe katika maisha yako yote.
Tukirudi katika maisha ya kawaida, ndani ya jamii zetu jamani watu tunapenda kusifiwa kwa yale makubwa na mazuri  tunayoyafanya. Au sivyo ndugu yangu? Eeeeh hata kwa yale madogo pia!!!!!!!

Basi tukirudi kwa Mungu wetu ni zaidi tena mno. MUNGU anapenda kutukuzwa na biblia inasisitiza kuwa “ katikati ya sifa Mungu ndio hushuka”. Lakini pia kuna njia nyingi ambazo watoto wa Mungu hupaswa kuzitumia katika kumsifu yeye. Nazo ni zipi?

“Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake. Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake. Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi; Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi; Msifuni kwa matoazi yaliayo; msifuni kwa matoazi yavumayo sana. Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya”. Zaburi 150
Katika kitabu hiki cha Zaburi tumeona mbinu mbalimbali, sababu nyingi na mahali ambapo tunatakiwa kumsifu Mungu.

Wengi watajiuliza maswali, Ni kwa nini tumpe Mungu sifa. Mungu akipewa sifa na akafurahi, hapo utupatia watu wake nguvu katika kushinda yale yanayotukabili katika maisha yetu. Kwa sababu Mungu akitutendea yaliyo mema inatupasa turudi kwake kwa ajili ya kumshukuru na hapo Mungu huona kuwa unatambua uweza wake na nguvu alizonazo hivyo basi atazidi kukuinua siku hadi siku katika maisha yako!

Hata wanadamu wakipewa sifa ndipo huzidisha juhudi katika kutenda yaliyo mazuri. Lakini kwa Bwana wetu Yesu kristo ni tofauti na wanadamu kwa sababu yeye hana ubaguzi hivyo humpatia kila mmoja kwa nafasi yake.

“Kwa kuwa furaha ya Bwana ni NGUVU zenu”. Nehemia 8:10b…………….. hivyo ndugu yangu tuzidi kumfurahisha Mungu wetu ili azidi kutuongezea nguvu katika maisha yetu.
Na kwa kumalizia tuone njia zingine za kumsifu Mungu, sio kwa kuimba tu, ama kucheza bali hata kwa
1.      Kwa matoleo [dhabihu za kushukuru ama sadaka ya shukrani]………………………Zaburi 50:23
2.      Kwa kumtumikia kikamilifu, mf; usafi kanisani, ujenzi wa kanisa yani shughuli zote za kikanisa kwa ujumla……………………….Zaburi 100:1,2
3.      Kwa njia ya maombi pia tunaweza kumsifu Mungu, na hapa wengi hukosea wakiamini kwenye Maombi ni wakati wa kueleza shida zao tu. La hasha tunatakiwa kufanya Maombi kwa ajili ya kumsifia Mungu wetu.

Mf. “ Mungu, wewe ni baba yetu, wewe ni Mungu uliyetukuka, ni Mungu wa kushinda wala hujui kushindwa na hujawahi kushindwa, umeoneka kuwa mwema katika maisha yangu siku hadi siku, na ndio maana sitoacha kukusifu katika yangu. Mungu wangu wewe ni mzuri, uzuri wako hako wa kuufananisha nao, maana wewe ni wa tofauti katika maisha ya wanadamu una upendo wa pekeee, haubagui ………………………………..” 
Huo ni mfano wa namna tunavyoweza kumsifia Mungu wetu kwa njia ya Maombi

Tunachotakiwa sasa nikumuahidi baba yetu wa Mbinguni kumsifu kweli katika maisha yetu yote ili nay eye aweze kutushindia. Haleluya watumishi wa Mungu……….
Basi tutasoma vitabu vifuatavyo kisha tutakuwa tumeweza kumuahidi Mungu kumrudishia sifa na utkufu wake. Zaburi 71:14,  71:8 na Zaburi 34:1

Na Mungu awabariki.

UPENDO


Jina la Yesu  lipewe  sifa………..

Nakupenda sana msomaji wa ukurasa huu wa NUKUU ZA MUNGU
Na wewe ni mtu wa pekee sana kwangu, natambua uwepo wako katika kushirikiana nami kutangaza Neno la Mungu.

Hivyo basi nahitaji kushirikiana na wewe leo neno linahusu UPENDO!
Upendo huwezi kutokea pasipo kuonesha ama kutambua thamani ya kile ukipendacho. Hivyo upendo ni hali ya kuonesha kujali, kuthamini kitu ama MTU.

Upendo ni agizo tulilopewa na Mungu, na kuthibisha hili Mungu alianza kutupenda sisi. “ Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe pekee, ili kila mtu mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”. Yohana 3:16

Hii ni dhahili kabisa kuwa UPENDO ni kitu chenye thamani kinachoweza hata kugharimu uhai wa mtu. Lakini basi, ni nani awezae kuufuata ule UPENDO aliotuonesha bwana Yesu kwa kukubali kujitoa uhai wake kwa ajili ya maisha yetu? Jibu ni hakuna……….sio mimi nasema bali  “Hakuna aliye na upendo mwingi kama huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.” Yohana 15:13

Hivyo basi Mungu kwa kutambua madhaifu yetu na mapungufu yetu ametuagiza kupendana sisi kwa sisi, kuchukuliana mizigo, kusaidiana matatizo kuona kila mmoja anathamani kwa mwenzie, na hapo tutakuwa tunampenda Mungu. Kwani katika kitabu cha 1 Yohana 4:21 tunaagizwa “Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye mungu, ampende na ndugu yake.” Hii inamaanisha kuwa mtu hawezi kumpenda Mungu kama hajampenda ndugu yake kwanza.

Na humohumo kwenye biblia inaongeza kwa kutuulizaa, Kama unaamchukia ndugu yako unaye muona, Je,  Mungu usiye muona utampendaje? Hivyo upendo uanze kwetu sisi wenyewe.

Warumi 12:9, inasisitiza kuwa upendo wetu usiwe wa kinafki, tupendane UPENDO wa kweli kwani pendo la kweli lina faida, linajenga Amani,  linaondoa Uongo, linaleta Baraka, LINAONDOA DHAMBI.
Na katika UPENDO tutafika mbinguni, kwani utatuweka karibu na Mungu na kutuweka mbali na dhambi.

Siku njema, na Mungu akubariki kwa Upendo wake wa kweli.


Jumatatu, 27 Aprili 2015

TUTAMBUE MAHALI SAHIHI PA KUELEZA SHIDA ZETU.



Habari za wakati huu,  ndugu msomaji katika ukurasa huu wa NUKUU ZA MUNGU.

Leo naanza kwa maswali mawili matatu hivi;

1.      Je unajua mahali sahihi pa kueleza shida zako?
2.      Je ni nani wakumueleza shida zako?
3.      Ipi ni njia sahihi ya kumaliza shida zako?

Wengi wamekuwa wakikosa majibu ya maswali haya, na kuanza kuhamisha imani zao kwa kupeleka shida zao kwa ndugu, majirani na wengine hata kudiriki kwenda kwa waganga wakiamini kupata suluhisho ya maswali yao.

Lakini leo nataka kuwapa jibu lililo sahihi ambapo tukianza kwa kuangalia katika kitabu cha Marko 11:24 “Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, amini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.”

Hivyo basi ndugu msomaji tunaelezwa kuwa kuwa NJIA iliyo sahihi yakueleza shida, mahitaji na matatizo yetu ni kwa njia ya MAOMBI, KUFANYA SALA kwa baba yetu yetu aliye MBINGUNI. Na si kama vile watu wanavyofikiri kueleza matatizo yao kwa ndugu ama kwa majirani na wengine kwenda kwa waganga.

Hiyo sio njia sahihi ndugu zangu, leo tunajifunza hili ili tupate kujua kuwa Mungu ndio msuluhishi wa matatizo yetu na sio mtu mwingine yeyote.

Mathayo 7:7 “Ombeni nanyi mtapewa, tafuteni mtaona, bisheni nanyi mtafunguliwa.”  
  • ·         Wewe unaomba kwa nani?
  • ·         Unatafuta kwa nani?
  • ·         Unabisha kwa nani?
Ili kupata muafaka wa mahitaji yako?

Mungu wetu hashindwi na jambo Bwana, ebu nenda wazungu wanasema direct kwake mueleze mambo yako, muombe mahitaji yako, tafuta kwake kilicho chako, kapate haki yako.

Zungumza naye kwa upole, kuwa na ujasiri katika kumueleza mambo yako, naye atakujibu. Halleya!!!!!!!!!!!!!!!!!

Wengi wetu tunaharibu wenyewe, pasipo kujua. Tunahitaji Mungu atujibu mahitaji yetu huku mioyoni mwetu tumebeba mizigi isiyo mpendeza Mungu,  TUJIULIZE SISI KAMA WANADAMU NA KAMA MZAZI, MTOTO WAKO AMEKUKOSEA,  JE MTOTO  ATAPATAJE UJASIRI WAKUELEZA SHIDA ZAKE KWA MZAZI?

Na sisi kwa Mungu wetu ni watoto wake, tunapomkosea hukasirika sana. Hivyo tunakiwa kuomba msamaha ama kutubu dhambi zetu kabla ya kueleza shida zetu.

NDUGU MSOMAJI TUNACHOTAKIWA KUFAHAMU NI NAMNA YA KUENDENDA SAWASAWA MBELE ZA MUNGU, NAYE NI MWEMA KATIKA MAISHA YETU, ANASIKILIZA NA KUJIBU MAOMBI YETU. HIVYO TUJINYENYEKEESHE MBELE ZAKE NAYE ATATUJIBU.

BASI NIKUTAKIE WAKATI MWEMA WENYE BARAKA ZA MUNGU…………….
NATUKUTANE SIKU NYINGINE


Alhamisi, 16 Aprili 2015

MSAMAHA NI DAWA KATIKA MAISHA YETU



Habari za wakati huu ndugu msomaji wangu,
Na, Bwana Yesu apewe sifa!

Leo tunaenda kujifunza juu ya MSAMAHA
Kwanza kabisa tupate kufahamu MSAMAHA ni kitu gani?  “Neno  SAMEHE” linamaanisha kusafisha nia au jambo nakulifanya kutokuwa na mawaa yoyote, ku achilia, kufuatilia mbali deni”.
Tunapokosea mtu uhuliza msamaha wake ili kurudisha uhusiano. Hapa tunaona kuwa msamaha huleta upendo, huruma na neeema. Msamaha ni jambo la hiari mtu hutakiwi kulazimishwa kutoa msamaha.
Neon la Mungu linatuhitaji sisis wanadamu kuwasamehe wenzetu pale wanapotukosea, haijalishi ni kosa la namna gani amekufanyia. Ila cha kushangaza wanadamu wa leo hatujui kusamehe bali tunabaki kuhesabiana makosa ya watu waliokusea.

[ Mambo ya Walawi 19:18], “usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yakokama nafsi yako; Mimi ndimi Bwana…….
Biblia inatuonyesha vitu vinavyopelekea kukosekana kwa msamaha ni kinyongo na chuki juu ya mtu mwingine. Lakini Mungun kupitia biblia bado anatu onya tusifanye visasi kwa ndugu zetu, jirani zetu na hata watu wote wanaotuzunguka.
Kutoa msamaha kwa walio tukosea ni Hazina kwetu siku ya mwisho tukikutana katika makao ya milele mbinguni. Wengi hukata tamaa ya kusamehe wengine kwa kuwahesabia idadi ya makosa walioyatenda, bali Mungu anatuelekeza kuwa Tusichoke kutoa misamaha kwa waliotukosea hata kama wametukosea mara Elfu na Elfu. “ Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikosea mara ngapi name nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.       [ Mathayo 18:21, 22].

Na tujiulize maswali kadhaa juu ya faida na hasara  tutakazo zipata baada ya kutoa ama kutokutoa masaha kwa wengine?     “ Kwa maaana mkiwasamehe watu makosa yao, na baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe ninyi  watu makosa yao, wala baba yenu hatawasemehe ninyi makosa yenu.” [ Mathayo 6:14, 15]

Maisha yetu tunaanza kuyatengeneza tukiwa hapahapa Duniani, kwa maana mtun akipandacho ndicho atakachon kujan kukivuna. Hivyo ndugu zangu wakristo tujifunze kutoa misamaha kwa wengine ndipo na Baba yetu wa mbinguni atatusamehe na sisi makosa yetu.

Mungu hawezi kutusamehe, kama sisi hatuwezi kuwasamehe wengine. “ Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako”    [ Isaya 43:25], na tuvae ule upendo wa Mungu kwetu, kwani Mungu akisamehe huwa hatkin kukumbuka yale tuliyo mkosea. Bali sisis binadamu tumezoea kutoa msamaha kwa kusema “ Nimekusamehe ila sitokusahau” , Mungu hapendi hivyo. Tukisamehe tuachilie na kusahau ndani ya mioyo yetu.

Msamaha utatusaidi kupata mafanikio ya Kiroho na Kimwili pia, kwani msamaha huleta Amani, Upendo, Baraka na Neema katika maisha yetu yote kiujumla.

Na Mungu akubariki, 
Tukutane wakati mwingine wa Mungu.